Manabii walionya watu wa Mungu kuhusu hukumu kwa dhambi zao, lakini pia waliwaambia kuhusu huruma na msamaha wa Mungu kwa watu waliotubu na kumwamini. Waliwakumbusha kuhusu Mwokozi ambaye Mungu aliyekuwa amehidi zamani. Walisema, “Kuna Mmoja ambaye anakuja kuwaokoa kutoka kwenye dhambi zenu.”
Nabii Isaya alisema kwa Wayahudi, “Bwana mwenyewe atakupa ishara: bikira atamzaa mwana. Atamwita Immanueli, maana yake ‘Mungu pamoja nasi.’ Ataitwa Mfalme wa Amani. Enzi yake haitakuwa na mwisho kamwe.” Pia alitabiri kuhusu Mwokozi huyu kama mtumishi, kwamba atateseka na kudharauliwa, ambaye ataadhibiwa kwa ajili ya dhambi zetu. Lakini manabii walitabiri kwamba Mwokozi atafufuka. Na pia walitabiri vitu vinginevyo ambavyo vitamfanyikia Mwokozi. Kwa mfano, Mikono na miguu kudungika, kuuzwa kwa shilingi thelathini, kusalitiwa na rafiki, kuhesabiwa pamoja na wenye dhambi, n.k.
Manabii waliongea kuhusu Agano Jipya ambalo lingetimilia katika Mwokozi aliyeahidiwa. Mungu alisema kupitia nabii Yeremia, “Watu wangu walivunja agano langu lakini nitafanya agano jipya nao. Nitawatoa katika utumwa. Nitaweka sheria yangu katika akili zao na kuiandika kwa mioyo yao. Nitakuwa Mungu wao na watakuwa watu wangu.”
Mungu alimwambia nabii Ezekieli pia kitu kama hicho akisema, “Nitawapatia moyo mpya na kuweka roho mpya ndani yenu. Nitaondoa kutoka kwenu moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama . Nitaweka Roho wangu ndani yenu na kuwafanya kufuata maagizo yangu na kuwa waangalifu kutii amri zangu.
Baada ya watu wa Mungu kurudi Yerusalemu kutoka utumwani Babiloni, na baada ya kujenga Yerusalemu na hekalu, Mungu alisimama kuongea kupitia manabii kwa miaka mia nne. Lakini katika wakati huo wa mateso, bado Wayahudi wengine walikumbuka ahadi za Mungu kuwaletea Mwokozi.
| Ushairi wa Ahadi |
Unabii |
Ushairi wa Kutimiza |
|
Isaya 9:7 |
Atarithi kiti cha enzi cha daudi |
Mathayo 1:1 |
|
Mika 5:2 |
Pahali pa kuzaliwa kwake |
Mathayo 2:1 |
|
Danieli 9:25 |
Mzaliwa atakapozaliwa |
Luka 2:1-2 |
|
Isaya 7:14 |
Nani atakayemzaa |
Mathayo 1:18 |
|
Yeremiah 31:15 |
Watoto wengi watauwawa |
Mathayo 2:16 |
|
Hosea 11:1 |
Kutoroka kwake hadi Misri |
Mathayo 2:14 |
|
Isaya 9:1-2 |
Kazi yake katika Galilaya |
Mathayo 4:12-16 |
|
Zaburi 110:4 |
Yeye ni kuhani kama Melkizedeki |
Waebrania 6:20 |
|
Isaya 53:3 |
Atakataliwa na Waisraeli |
Yohana 1:11 |
|
Isaya 11:2 |
Baadhi ya tabia zake |
Luka 2:52 |
|
Zakaria 9:9 |
Anakuja katika Yerusalemu |
Mathayo 21:1-11 |
|
Zaburi 41:9 |
Alisalitiwa na rafiki |
Marko 14:10 |
|
Zakaria 11:12-13 |
Vipande thelathini vya fedha vililipwa |
Mathayo 26:15 |
|
Zaburi 27:12 |
Mashahidi wa uwongo walimshtaki |
Mathayo 26:59-62 |
|
Isaya 53:7 |
Alinyamaza aliposhtakiwa |
Mathayo 26:62-63 |
|
Isaya 50:6 |
Alipigwa na kutemewa mate |
Marko 14:65 |
|
Zaburi 69:4 |
Alichukiwa bila sababu |
Yohana 15:23-25 |
|
Isaya 53:4-5 |
Aliumia kwa ajili ya wengine |
Mathayo 8:16-17 |
|
Isaya 53:12 |
Alisulubishwa kati ya wenye dhambi |
Mathayo 27:38 |
|
Zaburi 22:16 & Zakaria 12:10 |
Mikono yake na miguu ilidungwa |
Yohana 20:25-27 & Yohana 19:37 |
|
Zaburi 22:6-8 |
Alithihakiwa na kutukanwa |
Mathayo 27:39-44 |
|
Zaburi 69:21 |
Alipewa siki kunywa |
Yohana 19:29 |
|
Isaya 53:12 |
Anawaombea maadui wake |
Luka 24:34 |
|
Zaburi 22:18 |
Walilichezea kamari vazi lake |
Marko 15:24 |
|
Zaburi 16:10 |
Anafufuka kutoka kwenye wafu |
Luka 24:1-8 |
|
Zaburi 68:18 |
Anapaa Mbinguni |
Luka 24:50-51 |
|
Mwanzo 12:3 |
Kupitia kwake makuja Baraka aliyoahidiwa Abrahamu |
Wagalatia 3:14-29 |