Book of Acts

Swahili Stories

Uponyaji wa Ombaomba Kilema

Matendo 3:1-26

Siku moja, Petro na Yohana walikuwa wakienda Hekaluni kusali saa ya kusali, wakakutana na mtu kiwete. Mtu huyu alikuwa kiwete tangu kuzaliwa na alichukuliwa kila siku hadi kwenye lango la Hekalu lililoitwa Mzuri ili kuomba kutoka kwa wale wanaokwenda Hekaluni. Alipowaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni, aliwaomba fedha. Petro na Yohana wote wakamtazama mtu huyo, naye Petro akasema, “Tutazame sisi.” Yule mwombaji kiwete akawatazama, akitarajia kupokea kitu kutoka kwao, lakini Petro akasema, "Sina fedha na dhahabu, lakini nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende." Petro akamshika mkono wa kuume yule kiwete, akamwinua, na mara miguu yake ikapata nguvu. Naye akaruka, akasimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia hekaluni pamoja nao, akitembea, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu! Watu wakamwona akitembea na kumsifu Mungu, wakamtambua kuwa ndiye aliyekuwa ameketi kwenye lango la Hekalu akiomba fedha. Nao wakajawa na mshangao na kustaajabia yaliyotokea.

Petro akauambia ule umati wa watu, “Mbona mnastaajabu kana kwamba tulifanya hivi kwa uwezo wetu wenyewe, wakati uweza wa Mungu uliokuwa ukimtukuza Mwanawe Yesu? . . . Ninyi mlimwua Yesu, aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Sisi ni mashahidi wa jambo hili. Na ilikuwa kwa imani katika jina la Yesu huyu mtu huyu mnayemjua alitiwa nguvu.

Kisha akaeleza maandiko kuanzia kwa Ibrahimu katika maisha, kifo, na ufufuo wa Yesu Kristo. Kisha akasema, Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.