Book of Acts

Swahili Stories

Mitume Mbele ya Baraza la Wayahudi

Matendo 5:12-42

Baada ya kifo cha Anania na Safira, mitume waliendelea kufanya ishara na maajabu mengi. Walikuwa wakikutana mahali pa kukutania kando ya Hekalu, na waumini wengi waliongezwa kwenye hesabu yao, wanaume kwa wanawake. Watu wengi walikuwa wakitoka katika miji ya jirani wakiwaleta wagonjwa na wenye pepo, hata wakiwaweka katika mikeka barabarani ili kivuli cha Petro kiwapite alipokuwa akipita. Na wote wakaponywa.

Wakati huo kuhani mkuu akasimama pamoja na Masadukayo, wakajaa wivu, wakawakamata mitume na kuwaweka gerezani. Lakini wakati wa usiku malaika wa Bwana alifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akisema, "Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu." Na waliposikia, waliingia Hekaluni kulipopambazuka, wakaanza kufundisha.

Kuhani mkuu na baraza la Wayahudi walipokusanyika siku iliyofuata waliwaita mitume waletwe kwao.Hawakuwakuta gerezani, ingawa walinzi walikuwa pale na milango imefungwa. Walichanganyikiwa sana ripoti ilipowafikia ikisema kwamba mitume walikuwa hekaluni wakifundisha wengine. Askari wakaenda na kuwaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa kupigwa mawe na watu.

Wakati huo Kuhani Mkuu akawauliza, akisema, Tuliwaagiza sana msifundishe kwa jina hili, lakini hapa mmejaza mafundisho yenu Yerusalemu, na mnatupa hatia kwa ajili ya damu ya mtu huyu.

Petro akamjibu, "Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu ambaye ninyi mlimwua kwa kumtundika juu ya mti. Mungu alimkweza mkono wake wa kuume, awe kiongozi na Mwokozi, awape Israeli toba na msamaha wa dhambi. Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wanaomtii."

Waliposikia hivyo walikasirika na kutaka kuwaua. Wakati huo Mfarisayo mmoja na mwalimu aitwaye Gamalieli alisimama na kuzungumza na Baraza la Kiyahudi baada ya kuwaweka nje mitume. Aliwakumbusha kuhusu watu wengine walioinuka wakidai kuwa ni Masihi na jinsi kila harakati zao zilivyofeli. Kisha akawaonya viongozi wengine, akisema, “Jiepusheni na watu hawa, kwa maana ikiwa shauri hili ni la mwanadamu, litashindikana; lakini ikiwa limetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwaangusha, hata mkaonekana kuwa mnampinga Mungu.

Baraza lilichukua ushauri wa Gamalieli, likawaita mitume ndani na kuwapiga, na kuwaamuru wasiseme kwa jina la Yesu.

Mitume wakatoka nje ya baraza, wakishangilia kwa kuwa wamehesabiwa kuwa wamestahili kuaibishwa kwa ajili ya Jina la Yesu. Kisha wakaendelea kufundisha na kuhubiri kwa jina lake katika hekalu na pia nyumba kwa nyumba.