Book of Acts

Swahili Stories

B. Ushirika wa Waumini

Matendo 2:42-47

Muktadha:

Kwa kuja kwa Roho siku ya Pentekoste, Petro alihubiri kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Watu wengi walitubu na kubatizwa. Jambo lingine ambalo Petro aliwaambia akiwaonya lilikuwa hili. “Jiokoeni na kizazi hiki kifisadi.”

Hadithi hii ni jinsi watu katika kanisa la kwanza, hiki “kizazi kipya,” waliishi pamoja:

Maneno haya, “Jiokoeni na kizazi hiki cha sasa” yangewezaje kutusaidia kuelewa kifungu hiki kuhusu ushirika wa waumini?

  • Kizazi " ni utamaduni mzima . Kila kizazi - kina sifa zake za kawaida za kufikiria na tabia ..
  • Kwa hiyo jambo kuu linaloathiri akili na mioyo yao halipaswi tena kuwa roho ya nyakati, bali roho na kweli ya Mungu.
  • Kanisa lenyewe ni "kizazi kipya" - watu wapya kabisa , utamaduni mpya. Kanisa linapaswa kuonyesha ulimwengu njia mpya kabisa ya kuishi kama wanadamu chini ya Ubwana wa Kristo.

Na hadithi hii ni jinsi watu katika kanisa la kwanza, hiki “kizazi kipya,” waliishi pamoja:

HADITHI:

Walidumu katika mafundisho ya mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali. Watu wote wakaingiwa na hofu, na maajabu mengi na ishara zikafanywa na mitume. Waumini wote walikuwa pamoja na walikuwa na kila kitu shirika. Wakiuza mali zao na vitu vyao, wakampa mtu ye yote kadiri alivyokuwa na haja. Kila siku waliendelea kukutana pamoja katika ua wa hekalu. Wakamega mkate nyumbani mwao, wakala pamoja kwa furaha na moyo mweupe, wakimsifu Mungu na kupata kibali cha watu wote. Na Bwana akawazidishia hesabu kila siku wale waliokuwa wakiokolewa.